Please use this identifier to cite or link to this item: https://repository.seku.ac.ke/handle/123456789/8049
Title: Ontolojia ya nafsi katika riwaya teule za Muhammed Said Abdulla: Uchunguzi wa kikani
Authors: Khamis, Tatu Y.
Jumanne, Arafa
Keywords: Kani
Nafsi
Ontolojia
Issue Date: 2024
Publisher: South Eastern Kenya University
Citation: Dira ya Lugha, Juzuu 1, Na. 1, 70-80, 2024
Abstract: Makala hii inajadili ontolojia ya nafsi katika riwaya teule za Muhammed Said Abdulla kwa kujiegemeza katika kipengele cha kani. Kimsingi, kila mwanadamu ana nafsi. Nafsi ni kipengele kinachotazamwa kama uhai, roho pamoja na moyo (Kaponda, 2018). TUKI (1981) wanafasili dhana ya nafsi kuwa ndiyo roho au kiini cha dhati ya jambo husika. Hivyo, nafsi huongoza hali ya kupumua na kuupa uhai mwili wa mwanadamu. Aidha, kila nafsi inaongozwa na kani ambayo aghalabu huwa ni fiche. Data za msingi zilizofafanuliwa katika makala hii zimepatikana maktabani na uwandani kwa kutumia mbinu ya usaili na uchambuzi wa maandiko. Nadharia ya Nje- Ndani ilitumika katika kuongoza mjadala. Matokeo ya mjadala yanaonesha kuwa nafsi kiontolojia haiwezi kuonekana lakini kani yake inabainika katika matendo, lawama, kupaparika, kutulia na kuamrisha maovu. Ithibati ya matokeo haya yametolewa kutoka katika riwaya tatu za Muhammed Said Abdulla ambazo ni Duniani Kuna Watu, Kosa la Bwana Msa, na Kisima cha Giningi.
URI: https://jadilu.seku.ac.ke/index.php/jadilu/article/view/27/33
http://repository.seku.ac.ke/xmlui/handle/123456789/8049
ISSN: 3079-3882
Appears in Collections:School of Humanities and Social Sciences (JA)

Files in This Item:
File Description SizeFormat 
Khamis_Ontolojia ya nafsi katika riwaya teule za Muhammed Said Abdulla....pdfabstract3.68 kBAdobe PDFView/Open


Items in DSpace are protected by copyright, with all rights reserved, unless otherwise indicated.