Please use this identifier to cite or link to this item: https://repository.seku.ac.ke/handle/123456789/8104
Title: Usawiri wa wahusika wa kiume katika riwaya ya chozi la heri
Authors: Kiema, Agnes M.
Mutua, John
Ngesu, Sarah N.
Keywords: sawiri
wahusika
uhalisia
jinsia
nadharia
fasihi
Issue Date: 1-Jul-2025
Citation: European journal of linguistics, volume 4, issue 2, pp 41-48, 2025
Abstract: Makala hii imechunguza, usawiri wa wahusika wa kume katika riwaya ya Chozi la Heri(2017). Katika ulimwengu wa riwaya ya Kiswahili na fasihi, imekuwa kama jambo la kawaida kuona watafiti wengi wakichunguza masuala ya wanawake zaidi kuliko masuala ya wanaume. Jambo hili limetokana na ukweli kwamba, wanawake wamekuwa wakipiganiwa haki zao ili kuwafanya sawa na wanaume katika nyanja mbalimbali za maisha. Atieno(2019) anaeleza kuwa, kupuuzwa kwa jinsia ya kiume kumechangia hali yao ya upweke, kwani hakuna anayewafikiria wala kuwatetea kama inavyofanyiwa jinsia ya kike. Riwaya hii imeteuliwa kimakusudikwa sababu inamsawiri mhusika wa kiume katika nyanja mbalimbali za maisha. Makala hii iliogozwa na nadharia ya uhalisia.Nadharia ya uhalisia inadai kwamba, fasihi inatakiwa kutoa picha halisi ya jamii husika.Nadharia hii ilizuka huko Ulaya katika karne ya kumi na tisa.Utafiti huu ulifanyika maktabani ambapo riwaya ya Chozi la Heriilisomwa na kuhakikiwa. Ni matumaini yetu kuwa, Makala hii imetoa mwanga mkubwa kuhusiana na masuala ya jinsiaya kiume. Aidha, Makala hii itakuwa kichocheo cha watafiti wa baadaye wa fasihi kuchunguza masuala yanayohusu jinsia ya kiume
URI: https://carijournals.org/journals/index.php/ejl/article/view/2879/3243
http://repository.seku.ac.ke/xmlui/handle/123456789/8104
ISSN: 2957-4641
Appears in Collections:School of Humanities and Social Sciences (JA)

Files in This Item:
File Description SizeFormat 
Kiema_Usawiri wa wahusika wa kiume katika riwaya ya chozi la heri.pdfabstract4.5 kBAdobe PDFView/Open


Items in DSpace are protected by copyright, with all rights reserved, unless otherwise indicated.